Sunday, 15 July 2012 17:39
Mgomo Wa Madaktari Gertrudes Wasitishwa
Sasa imebainika kuwa kenya inakumbwa na upungufu wa zaidi ya madaktari 37,000 huku hospitali nyingi humu nchini zikiendelea kushuhudia visa vingi vya wagonjwa wanohitaji matibabu maalum. haya ni kwa mujibu wa muungano unaotetea maslahi ya madaktari na wauguzi, kmpdu ambao pia umetangaza kusitishwa kwa mgomo wa madaktari wapatao 24 wa hospitali ya kibinafsi ya gertrudes waliogoma tarehe 9 mwezi uliopita.




















